Breaking News

Aweso awafunda Maafisa Manunuzi


Na Hellen Mtereko, Mwanza

Maafisa manunuzi wa Mamlaka za Maji  Nchini wametakiwa kufanya kazi kwa ushirikiano hali itakayosaidia kurahisisha utekelezaji wa miradi ya maji kukamilika kwa wakati.

Rai hiyo imetolewa leo Desemba 13,2021 na Waziri wa Maji  Mhe. Jumaa Aweso wakati akifungua kikao cha Maafisa Manunuzi wa Mamlaka ya Maji kilicho lenga kujadili utendaji kazi ambacho kimefanyika Jijini Mwanza.

Maafisa Manunuzi wakiwa kwenye kikao kilicho lenga kujadili utendaji kazi

Amesema kuwa ili maafisa Manunuzi waweze kufikia kwenye malengo mbalimbali waliyojiwekea wanapaswa wafanye kazi kwa bidii, wawe na nidhamu kazini pamoja na ushirikiano.

"nitoe wito kwa  baadhi ya Maafisa Manunuzi mjitahidi sana kukamilisha utaratibu wa Manunuzi ili shughuli ziwe zinatekelezwa kwa wakati, mnapo  chelewa   kwa kigezo cha kufanya mchakato wa Manunuzi usio kamilika mnasababisha  miradi kushindwa kukamilika kwa wakati",amesema Aweso

Kwa upande wake Afisa Manunuzi kutoka Luwasa  Korogwe, Halima Mhando amesema kuwa ameyapokea maelekezo yote yaliyotolewa na Waziri wa Maji ikiwemo kufanya kazi kwa ushirikiano ili kuweza kuhakikisha kazi za kutekeleza miradi  zinasonga mbele.

Mwishoooo

No comments