Breaking News

WAJAWAZITO WATAKIWA KUANZA KLINIKI MAPEMA KUEPUSHA VIFO

 Na Tonny Alphonce,Mwanza

Wajawazito wametakiwa kuanza kliniki mara moja pindi wanapobaini kuwa ni wajawazito kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kukabiliana na ongezeko la watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi.

Ushauri huo umetolewa na afisa maendeleo na ustawi wa jamiii wa chama cha wazazi wenye watoto wenye vichwa vikubwa na mgongo wazi Thelesia Jacob katika hafla iliyoandaliwa na aliyekuwa Miss Mwanza mwaka 2013 Lucy Charles yenye lengo la kushiriki chakula cha pamoja na watu wenye umelavu ili kusikilia changamoto zinazowakabili.

Akizungumza katika hafla hiyo Thelesia amesema kuna baadhi ya wajawazito hawazingatii taratibu na miongozo ya kuhudhuria kiliniki jambo linalosababisha madhara ikiwemo ya Watoto kuzaliwa wakiwa na tatizo la vichwa vikubwa na mgongo wazi.

‘Mama anapochelewa kuanza kliniki mapema anaweza kupata matatizo mbalimbali ya kiafya kwa upande wake na kwa mtoto na ndio maana wataalamu wa afya wanasisitiza mama aanze kuhudhuria kliniki mara baada ya kujigundua kuwa na ujauzito.alisema’

Kwa upande wake liyekuwa Miss Mwanza mwaka 2013 Lucy Charles amesema watu wenye ulemavu wanakabiliwa na changamoto nyingi hivyo kupitia taasisi yake ya Tabasam na Lucy Charles anakusudia kuwashika mkono ili na wao waweze kufikia ndoto zao.

‘Huu ni mwendelezo wa kazi zinazofanywa na taasisi yangu ikiwa ni sehemu ya kurudisha kile tunachokipata kwenye jamii na kuwa kuwarudishia tabasamu wale waliolipoteza kutokana na matatizo mbalimbali.alisema Lucy’

Kwasasa Mwanamitindo huyo pia ni muigizaji wa filamu na amesema kupitia jukwaa hilo anakusudia kuinua vipaji kupitita Sanaa ya maigizo.

Miongoni mwa watu wenye walemavu walioshiriki kwenye hafla hiyo Zainab Habibu na Habibu Mrope wameomba watu binafsi na mashirika mbalimbali kujitokeza kuwasaidia kwasababu bado wanakabiliwa na changamoto lukuki.

No comments