Breaking News

KEMEENI MILA NA DESTURI ZINAZOKANDAMIZA WATOTO WA KIKE

Joyce Joliga,Songea

Jamii imeshauriwa kukemea  Mila na desturi  potofu    ambazo zimepitwa na wakati wanafanyiwa watoto wa kike  ikiwemo kutopelekwa shule,kukeketwa na kufundishwa mafunzo yasiyofaa katika umri mdogo wa miaka 5-8,kwani vitendo hivyo ni vya ukatili na havifai kufumbiwa macho.


Wito  huo umetolewa wakati wa siku ya Mtoto wa kike duniani  na Mkurugenzi wa Faraja  toto ,Alfrida  Msemwa wakati akizungumza na mwandishi wa habari  ofisini kwake.

Alisema,jamii inapaswa kuwaangalia watoto wa kike kwa jicho la tatu ili waweze kufanikiwa kwenye elimu ,na maisha yao ya baadaye.

"Jamii inapaswa kuwathamini na kuwasaidia watoto  wa kike ,kwa kuwalea katika maadili mema, na kuwasaidia kupata elimu ili waweze kufanikiwa kutimiza ndoto zao ,"alisema Faraja

Aidha wazazi wametakiwa kuwajengea uwezo watoto  wa kujiamini na kusoma kwa bidii ili kuweza kutimiza ndoto zao pindi watakapokua wakubwa.

Naye Anna Gabriel  mkazi wa Namtumbo  amewashauri wazazi kutoa haki Sawa kwa watoto  wote bila upendeleo,na kuondokana na fikra potofu kuwa kumsomesha mtoto wa kike  ni kupoteza muda kitu ambacho si sahihi.

Kwa upande wake  mtaalam wa malezi na makuzi ya mtoto  Davis Gisuka ametoa ushauri kwa wazazi  na walezi kuendelea kuwalea watoto  kwa pamoja ikiwa ni pamoja na kuwathamini kwani watoto  wote nisawa.

Alisema,Katika jamii nyingi za kitanzania watoto wa kike wamekuwa wakipewa kazi nyigi sana za nyumbani kuliko wa kiume

Hali hii husababisha mtoto wa kike kukosa muda wa kujisomea kulinganisha na mtoto wa kiume..

Mwisho.


No comments