CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA NYANZA CHAANZA KUVUNA SAMAKI KWA NJIA YA VIZIMBA
Na Tonny Alphonce, Mwanza
Bi.
Boniphace amesema kuwa hatua hii ni kubwa na inaonyesha mafanikio licha ya
changamoto zilizopo kwenye ufugaji wa samaki kwa njia ya vizimba. Ameongeza
kuwa wengine wameshindwa kutokana na changamoto mbalimbali ikiwa ni pamoja na
wizi wa samaki, lakini chama cha Nyanza kimefanikiwa.
"Sasa
nyinyi ni wazoefu, mmeweza kuuendesha mradi huu wa vizimba vinne. Wengine
wamefeli njiani, wengine wamekuwa wakilalamika samaki wanaibiwa lakini Nyanza
mmeweza na sasa nyie sio wageni tena maana mnajua samaki wanahitaji nini, wapi
mnaweza kupata vifaranga vya samaki na wapi mtapata chakula cha samaki ni vema
mkaendelea kujiimarisha katika mradi huu," alisema Bi. Boniphace.
Amewataka
viongozi wa chama hicho kuangalia namna ya kuwekeza zaidi kwenye mradi huo kwa
kutumia fedha zitakazopatikana kupitia vyanzo vingine vya mapato.
Kwa upande
wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Chama kikuu cha Ushirika Nyanza, Leonard Lyabauma,
ameiomba serikali kuendelea kuwawezesha ili waweze kuendeleza mradi huo.
"Kwa
hivi sasa tumeanza kuvuna samaki, kina mama na vijana wameweza kupata samaki
kwa bei nzuri na kwenda kuwauza na hivyo kuunga mkono usemi wa serikali wa
uchumi jumuishi ambapo pande zaidi ya mbili zinanufaika kwa pamoja,"
alisema Bwana Lyabuma.
Chama kikuu
cha ushirika Nyanza ni miongoni mwa wanufaika na mkopo wa masharti nafuu
kupitia wizara ya kilimo na mifugo na walifanikiwa kuanza ufugaji wa samaki
katika vizimba vinne ambapo tayari wameanza kuvuna samaki hadi tani 30.
No comments