WANANCHI WALIPONGEZA JESHI LA POLISI MWANZA KWA KUWAOKOA WATOTO WAWILI WALIOTEKWA
Na Tonny Alphonce, Mwanza
Wananchi mkoani Mwanza wamelipongeza jeshi la Polisi mkoani
humo kwa kufanikiwa kuwaokoa watoto wawili wanafunzi wa shule ya Blessing
waliokuwa wametekwa na watu wasiojulikana wakati wakienda shule.
Wakizungumzia tukio hilo lililotekea tarehe 05/02/2025 wakati watoto Magreth Thobias (8) na Fortunatus Jophrey (5) walipotekwa wakati wakisubiria Bus la shule, wananchi hao wamesema jeshi la Polisi mkoani Mwanza linastahili pongezi kwa kuwa lilianza kufanyakazi usiku na mchana kuhakikisha watoto hao wanapatikana wakiwa hai.
Emmanuel Mlaki mkazi wa Mkolani mkoani Mwanza amesema
ushirikiano uliofanya kati ya wananchi na jeshi la Polisi unapaswa kuendelezwa
ili kukomesha vitendo vya uhalisi ambavyo vimekuwa vikitokea mkoani Mwanza.
Kamanda wa Polisi tumemsikia akisema jeshi la Polisi
limefanikiwa kuwaokoa hao watoto waliokuwa wamefichwa na watekaji katika mtaa
Nyarubugoya Nyegezi na tumewaona watoto wakiwa salama lakini watekaji wameuwawa
jeshi letu kwa kweli limefanya kazi kubwa sana na linastahili pongezi.alisema
Mlaki
Nae Suzan Kimaro mkazi wa Mtaa huo wa Nyarubugoya amesema
kila mwananchi anawajibu wa kuwalinda watoto kwa kuwa hawawezi kujipigania
wenyewe hasa wanapoenda shule na wakati wa kurudi nyumbani wanakuwa katika
hatari zaidi.
Sisi wanajamii tunatakiwa kuwa walinzi wa watoto wetu maana
wengine wanaenda shule kwa miguu na ikitokea unaona mtoto analia au anaomba
msaada jaribu kumsaidia maana huenda ndio wakawa watekaji wenyewe.alisema Susan
Tarehe 05/02/2025 watoto Magreth
Thobias (8) na Fortunatus Jophrey (5) walitekwa
wakiwa njiani kuelekea shuleni majira ya saa 12:30 asubuhi eneo la
Kapripoint mkoani Mwanza.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa
shirika la Dunia Rafiki Sophia Asenga amesema suala la usalama na ulinzi wa
mtoto ni la jamii nzima na kuwataka wananchi kuwalinda watoto popote wanapokuwa
kwa kuwa watu wenyenia mbaya wamekuwa wakiwatumia watoto ili waweze kujipatia
kipato jambo ambalo halikubaliki
Akidhibitisha kupatikana kwa
watoto hao ,kamanda wa Polisisi mkoani Mwanza
Wilbroad Mtafungwa amesema watoto
hao wamepatikana baada ya Polisi kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema na kifatilia hadi kwenye nyumba waliokuwa
wamehifadhiwa.
Kamanda Mtafungwa alisema polisi walipofika katika nyumba waliyokuwa wamehifadhiwa watoto hao na watekaji ambao majina yao hayakuweza kupatikana walianza kujihami kwa kutumia mapanga,nondo na jambia ndio polisi waliamua kutumia risasi za moto na kufanikiwa kuwaua pale pale.
Watoto Magreth Thobias na
Fortunatus Jophrey baada ya kuokolewa
walipelekwa katika hospitali ya Rufaaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou Toure kufanyiwa uchunguzi wa afya zao.
Programu Jumuishi ya Taifa ya
Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT- MMMAM) inasisitiza suala la
ulinzi na usalama wa mtoto ikieleza kwa upanda namna jamii na wazazi
wanavyopaswa kuwajibika katika suala la ulinzi na usalama wa mtoto huku mzazi
akitajwa kama mlinzi wa kwanza wa mtoto ambae atawajibika kuratibu mienendo
yote ya mtoto kuanzia asubuhi hadi usiku anapoenda kulala
No comments