Breaking News

MASHARTI YA CHANJO UVIKO-19 YAANZA KUWABANA WASAFIRI

 

Baada ya nchi mbalimbali kuchanja idadi kubwa ya watu wao chanjo ya corona, baadhi zimeanza kuweka masharti kwa wageni wanaoingia kuwa ni lazima wawe wamechanjwa dhidi ya virusi vya corona.

Nchi hizo sasa zimeanza kuweka masharti hayo kupitia baadhi ya mashirika ya ndege yanayobeba abiria, kuwa hawatakubali kumpokea raia yeyote ambaye hajachanjwa ili kudhibiti virusi hivyo kwenye nchi zao.

Hata hivyo Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetoa ufafanuzi kuwa hakuna sharti la chanjo ya corona kwa wasafiri wanaokwenda nje ya nchi.

Kaimu Mkuu wa Kitengo Cha Mawasiliano Serikalini-Afya, Catherine Sungura amesema ni vema msafiri akauliza shirika la ndege analokwenda nalo pamoja na masharti ya nchi anayotembelea.

“Kwa zile nchi ambazo zinahitaji kipimo cha Covid-19 msafiri afanye kipimo hicho ndani ya saa 24 hadi 48 kabla ya kuanza safari.

“Upimaji unafanyika kwa msafiri kufanya booking kupitia pimacovid.moh.go.tz ambapo atachagua kituo cha upimaji. Baada ya upimaji majibu yatatumwa kwake kwa njia ya barua pepe aliyotumia wakati wa booking. Akifika Airport cheti hicho kitahakikiwa katika dawati la afya. Unashauriwa kujiepusha na vyeti feki,” amesisitiza.

Waliokwama wafunguka


SOMA ZAIDI HAPA; CHANZO MWANANCHI

No comments