Breaking News

MKURUGENZI MTENDAJI WA NACOPHA ATAKA KUONGEZWA BAJETI YA MAPAMBANO DHIDI YA UKIMWI

Na Tonny Alphonce,Mara

Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI Bw Deogratius Rutatwa ameitaka Kamati ya Bunge ya masuala ya UKIMWI na Dawa za Kulevya kuongeza bajeti ya kupambana na ugonjwa wa UKIMWI.                       

Mkurugenzi Mtendaji wa Baraza la Watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI Bw Deogratius Rutatwa akitoa mchango wake mbele ya Kamati ya Bunge ya masuala ya UKIMWI na Dawa za Kulevya

Amesema Kwa Mkoa wa Mara kiasi kilichotengwa upande wa mwitikio wa UKIMWI ni asilimia 7 tu kiasi ambacho ni kidogo sana.                            

Bw Rutatwa amewaomba wabunge wa kamati ya UKIMWI kuishawishi serikali itenge fedha za kutosha Ili Taifa liweze kufika malengo ya sifuri tatu.                         

 Amewataka pia viongozi wa kisiasa na wataalamu kuwa makini kwenye matamshi yao kwa kuwa matamshi mengine yana wanyanyapaa Watu wanaoishi na VVU.   

"Unaposema kupatikana Kwa Virusi ya UKIMWI ni shida au tatizo hii itasababisha Watu kuacha kupima na hapo tutazidi kuongeza tatizo"alisema Bw Rutatwa. 

Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya masuala ya UKIMWI Bi Fatuma Hassan akiendesha kikao cha Kmati ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI na viongozi wa mkoa wa Mara.

kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya masuala ya UKIMWI Bi Fatuma Hassan amesema changamoto walizonazo watu wanaoishi na VVU mkoani Mara wamezisikia na kuutaka uongozi wa mkoa uangalia namna ya kutatua baadhi ya changamoto zinazowekana ikiwemo ya kupata mashine ya kupima uwingi wa virusi mwilini.                

Mkuu wa mkoa wa Mara Ally Salum Hapi akizungumza na wajumbe wa kamati ya masua ya UKIMWI na Madawa ya kulevya

Nae Mkuu wa Mkoa wa Mara Ally Salum Hapi ameihakikishia ushirikiano wa kutosha kamati hiyo kwa muda wote itakapokuwa mkoani humo.       

No comments