Breaking News

WADAU WA ELIMU NA WAZAZI WATAKIWA KUWEKEZA KATIKA ZANA CHANGAMSHI ZA WATOTO.

Na Tonny Alphonce,Mwanza

Wazazi na Serikali wametakiwa kuwekeza katika eneo la Uchangamshi kwa Watoto wadogo ili iwasaidie Watoto katika makuzi yao na kupata uelewa wa haraka katika mambo mbalimbali.

Kimsingi Watoto wadogo wanahitaji Uchangamshi na hivyo wanahitaji zana zitakazowasaidia katika kujifunza kwa haraka tofauti na mtoto ambae hatapitishwa katika eneo hili la Uchangamshi.

Kauli hiyo imetolewa na Mwl Alex Rwabigene ambapo amesisitiza suala la ubunifu wa Zana za kufundishia wasiachiwe walimu peke yao kwa kuwa suala la ubunifu ni zaidi ya suala la maelekezo na linatakiwa kutoka ndani ya moyo mwalimu husika.

‘tunachotakiwa kufanya sasa ni kuwatambua wabunifu wa zana hizi za Watoto ili wasaidie ubunifu wao uwasaidie walimu ambao sio wabunifu ili kuwa na zana muhimu za kuamsha uchangamshi kwa Watoto kwa kuwa tunaamini mazingira mazuri ya mtoto katika makuzi yake ya utoto ni muhimu sana na yanahusika kumfanya nani baadae.alisema Mwl Rwabigene.

Akizungumzia nafasi yake kama mbunifu wa zana za kufundishia Watoto, Mwl Rwabigene amesema kwa sasa Zana zao zimekuwa msaada mkubwa kwa baadhi ya shule na wazazi ambao wameanza kuzitumia na kupata matokeo mazuri.

‘Baadaya kuhangaika kwa muda mrefu kuielimisha jamii juu ya umuhimu wa Zana za kufundishia,sasa Zana zetu zimesambaa sana na ni baada ya serikali kuona umuhimu wetu katika eneo hili la Uchangamshi kwa Watoto na zana zetu zimesambaa katika maeneo mbalimbali kama Kagera,Tabora,Kigoma,Dar es Salaam na maeneo mengine wamekuwa wanaomba tuwatumie na wamekuwa wakikiri kuwa zana zetu zinawasaidia.Alisema Mwl Rwabigene.’

Mzazi akitengeneza Zana za kufundishia watoto kwa kutumia malighafi zinazopatikana kwa urahisi.

Akizungumzia mpango Jumuishi wa Malezi,Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto (MMMAM) Mwl Alex amesema mpango huo wa serikali kupitia Wizara ya Afya ni mkubwa na serikali imeonyesha dhamila ya dhati katika kulisukuma suala hili la kuwajengea msingi wa malezi Watoto kuanzia umri wa mwaka 0 hadi 8.

‘Malezi Jumuishi ya mtoto yana mambo mengi kuna habari ya Afya,Kuna habari ya Lishe,kuna habari Mahusiano,Malezi yao lakini pia kuna eneo la Uchangamshi na mpango huu umelibeba katika uzima wake kwamba Watoto wapate kutenda matendo,wapate kuchangamshwa wakianza katika umri mdogo,mambo yote hayo ndio yanamjengea hisia na kumfanya ukubwani kuwa mtu maalumu.alisema Mwl Rwabigene”

Bosco Bosco ambae ni mwanasaikolojia amesema suala la Uchangamshi kwa mtoto linaanzia pale mtoto anapokuwa tumboni ,hasa kipindi ambacho mtoto anaanza kucheza tumboni katika hatua hiyo anakuwa na uwezo wa kusikia na katika kipindi hicho baba na mama wanaweza kuanza kuongea na mtoto.

‘Wazazi wengi wanafanya makosa hawana tabia ya kuongea na mtoto akiwa tumboni na hata baada ya kuzaliwa,wengine wanadhani mtoto wa mwaka sifuri au miezi mitatu au mwaka mmoja haelewi ukimsemesha,sio kweli kitendo cha kumzungumza nae kinamfanya awe na hisia na uchangamfu kitu ambacho ni kikubwa sana katika ukuaji wa mtoto.alisema Bosco.’

Bosco amesema kitendo cha mlezi kutozungumza na mtoto au kuto kucheza nae kunaathiri ubongo wa mtoto kuchelewa kuku ana kutokuwa na uwezo wa kufikiri na kuchanganua mambo hata anapokuwa mkubwa.

Kwa upande wa Zana za kujifunzia Watoto Bw Bosco amesema mzazi anaweza kutumia vitu mbalimbali kama makopo,magome ya miti na vitu vingine ambavyo haviwezi kuleta madhara kwa mtoto na kwaajili ya kuchezea ambapo husaidia ubongo wa mtoto kuchangamka.

Mzazi Fredy Kabamba ambae ni mkazi Swea jijini Mwanza ambae ni mmoja wa wazazi ambaye amenunua Zana kwaajili ya mtoto wake mwenye umri wa miaka miwili na  nusu amesema zana hizo zimekuwa msaada mkubwa kwa Mtoto wake pamoja na mfanyakazi wake wa ndani kwa kuwa muda wote wamekuwa wakichezea zana hizo ambazo bila wao kujua zimekuwa zikijenga pia kiakili.

‘Mimi nilinunua zana za shilingi laki moja na nusu na nilivutiwa baada ya kupewa elimu kidogo na mwl Alex juu ya umuhimu wa Zana hizi kwa mtoto hasa katika eneo la Uchangamshi,dada wa kazi na mtoto wangu wamezipenda muda mwingi wamekuwa wakitumia kuunganisha maumbo mbalimbali pamoja na kupanga herufi na namba kwa usahihi,nimeona hata dada wa kazi imemsaidia maana hakubahatika kusoma kwa maana hiyo zana hizi zinamsaidia mtoto wangu na dada wa kazi.alisema Fredy’

Wadau mbalimbali bado wana nafasi ya kushirikiana na serikali katika kutekeleza mpango wa MMMAM kama ilivyo kwa SHIRIKA linaloangazia Malezi ,Makuzi na Maendeleo ya awali ya Mtoto (CiC ) ambalo kwa upande wake limefanikiwa kuongeza uwezo kwa walimu wa awali katika wilaya za Kongwa na Chamwino mkoani Dodoma kumudu mbinu za ujifunzaji na ufundishaji wa Elimu ya awali kutoka asilimia 50 Aprili, 2020 hadi kufikia asilimia 70 Disemba, 2020.

Nao Mwongozo wa Mwalimu wa kufundishia Elimu ya Awali unamuelekeza mwalimu  umuhimu utakaomsaidia kuboresha mchakato wa ufundishaji na ujifunzaji wa umahiri uliobainishwa katika mtaala na muhtasari wa Elimu ya Awali. Mwongozo huo umebainisha shughuli za kutenda mtoto ambazo zitamwezesha kujenga umahiri husika.

No comments