Breaking News

EMEDO YATAMBULISHA MRADI WA KUZUIA KUZAMA ZIWA VICTORIA ,RAS AWATAKA EMEDO NA WADAU KUISAIDIA SERIKALI

 Na Tonny Alphonce,Mwanza

Kutokana na kuongeza kwa shughuli za kiuchumi katika Ziwa Victoria wadau wametakiwa kuongeza jitihada za kuzuia ajali za wavuvi kuzama maji kwa manufaa ya mkoa na taifa kwa ujumla.

katibu Tawala Mkoa Wa Mwanza Elikana Balandya akifungua rasimi  kikao cha utambulisho wa Mradi Wa Kuzuia Kuzama Ziwa Victoria

Akizungumza katika utambulisho wa Mradi wa Kuzuia Kuzama Maji Ziwa Victoria unaotekelezwa na Shirika la Usimamizi wa Mazingira na Maendeleo EMEDO katibu Tawala Mkoa Wa Mwanza Elikana Balandya amesema mradi huo umekuja wakati pia serikali imeamua kuwekeza katika Ziwa Victoria  hivyo wadau hawana budi kushirikiana na serikali katika kuhakikisha uwekezaji huo unakuwa na tija.

“Kwa sasa Mkoa wetu wa  Mwanza Serikali inatekelezeka mpango wa BBT (Building Better Tomorrow) katika sekta ya ufugaji na uvuvi hivyo mradi wa kuzuia kuzama maji katika Ziwa Victoria utasaidia kutoa elimu ili kuzuia vifo zitokanavyo na kuzama maji na wananchi wataweza kufanya shughuli hizi za uvuvi kwa usalama”.alisema Balandya

katibu Tawala Mkoa Wa Mwanza Elikana Balandya akifungua rasimi  kikao cha utambulisho wa Mradi Wa Kuzuia Kuzama Ziwa Victoria

Kwa upande wake Arthur Mjema afisa mradi kutoka shirika la EMEDO amesema katika utekelezaji wake mradi utayagusa makundi manne ambayo ni Wavuvi,Watoto,kundi la kina mama wachakataji na kundi la nne kundi la vijana wasomba ngese.

Arthur Mjema afisa mradi kutoka shirika la EMEDO akiutambulisha mradi wa Kuzuia Kuzama Maji Ziwa Victoria kwa Wadau,hawapo pichani

Mgema amesema lengo hasa la kuyagusa makundio hayo ni kutokana na majibu ya utafiti ambayo yanaonyesha kuwa makundi hayo manne ndio makundi yaliyopo kwenye hatari ya kuzama maji.

Mkufunzi wa Chuo Cha Wanamaji Mwanza ASP Roberth Kelese ambae alipatiwa mafunzo ya uokoaji nchini Uingereza kupitia mradi huo akawataka wadau kuungana na EMEDO ili kuhakikisha mradi unafanikiwa.

Mkufunzi wa Chuo Cha Wanamaji Mwanza ASP Roberth Kelese akielezea mafunzo ya uokoaji waliyopatiwa nchini Uingereza

“Nilipokuwa Uingereza nimejifunza kuwa janga hili si lakuiachia taasisi moja peke yake lazima wadau tuungane ili kupambana na ajali hizi za majini ambazo kiukweli zinapoteza maisha ya watu wengi duniani kote”.alisema ASP Kelese.

Mradi huu wa kuzuia kuzama maji Ziwa Victoria  hadi sasa umeishatambulishwa katika mikoa yote mitatu ya mradi ,mkoa wa Mara,Kagera na Mwanza, ukiwa na lengo la kuhakikisha  hadi kufikia mwaka  2025 ajali za majini kwa wavuvi na wananchi wanaoishi pembezoni mwa ziwa Victoria zinapungua.


No comments