Breaking News

WAZAZI SHIRIKIANENI NA WALIMU WA AWALI KUTENGENEZA ZANA ZA KUJIFUNZIA WATOTO WA AWALI

 Na Joyce Joliga,Songea

Wazazi  kata ya Ruhuwiko Manispaa  ya Songea wameshauriwa kusaidiana na walimu wa madarasa ya awali kutengeneza Zana za kujifunzia watoto  wao ili kuwasaidia kuweza kujua kusoma,kuandika na kuhesabu kwa njia nyepesi zaidi,kwani vifaa hivyo havigharimu pesa yoyote vipo kwenye maeneo yao.



Wito huo umetolewa na Diwani kata ya Ruhuwiko Wilbard  Mahundi  wakati wa akizungumza na mwandishi wa habari  hii ambapo aliwataka kamati ya maendeleo ya elimu ya kata kuhakikisha inashirikiana na Wazazi  kujitolea kutengeneza  vifaa mbali mbali vya kujifunzia watoto kuhesabu kwa kutumia visoda,mabunzi, vijiti  Vizio vya soda ,kuchora  michiro mbalimbali ya wanyama,mimea, nyumba na hata matunda.


Alisema,Wazazi  wakishiriki kutengeneza  dhana za kujifunzi kutaleta hamasa kubwa kwa walimu na watoto wao hivyo siyo dhambi kama watashiriki kwenye zoezi hilo.


"Niwasihi sana wazazi wenzangu ambao tuna muda tujitokeze kusaidiana na walimu kutengeneza vifaa mbali mbali vya kujifunzia watoto wetu ili waweze kusoma kwa vitendo na kuelewa haraka,"Alisema Mh.Mahundi

Naye  Anna  Anosisye mkazi wa Ruhuwiko  alisema Kuna kila sababu wazazi kujitolea kutengeneza  Zana hizo kwani  zinawasaidia watoto  kupenda kwenda shule kujifunza kwa vitendo na wanaelewa zaidi tofauti  na kusoma tu.



"Watoto  wanavutiwa na mandhari nzuri za michiro  na uwepo wa Zana mbalimbali kwenye darasa unawasaidia kuwa making zaidi na masomo hivyo kupenda kujifunza zaidi."Alisema Anosisye

Naye Victor Maganga amewashauri  wazazi kupenda kufatilia na kuwekeza kwenye elimu za watoto  wao wa awali kwani ndio msingi imara wa maendeleo  ya mtoto na kuacha kuwaachia kila kitu walimu peke

Mtaala wa Elimu ya Awali umezingatia kwamba elimu bora ya awali ni muhimu kwa maisha ya mtoto. 

Mtoto akijenga msingi imara wa kujifunza katika Elimu ya Awali atakuwa tayari kuanza darasa la I na kuendelea vizuri katika ngazi zingine za elimu


No comments