Breaking News

MKUU WA WILAYA MAKILAGI - WAZAZI WASOMESHENI WATOTO KWA FAIDA YA BAADAE

 Na Tonny Alphonce,Mwanza

Wazazi na walezi wa wilayani Nyamagana mkoani Mwanza wametakiwa kuhakikisha wanawekeza katika elimu kwa watoto wao wakike na wakiume kwa manufaa yao na kwa taifa kwa ujumla.


Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Amina Makilagi akiongea na Wazazi na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mkuyuni ya jijini Mwanza.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Amina Makilagi wakati akizungumza na wazazi na walezi katika kikao cha kuwapongeza wazazi hao kwa kuwasomesha watoto wao katika shule hiyo ya Mkuyuni.

Mheshimiwa Makilagi amesema elimu pekee ndio inaweza kuwasaidia watoto kuwa na waisha mazuri ya baadae lakini pia ustawi wa taifa unategemea jamii iliyo elimika.

“Mzazi yoyote aliyewekaza katika elimu hawezi kulala njaa na atakula sasa hadi kufa kwake,elimu ni tofauti na biashara ambazo huanza na kufa tofauti na waliowekeza kwa Watoto ambao wanaendelea kuishi vizuri hadi sasa”.alisema Makilagi.

Makilagi amewataka wazazi kuhakikisha watoto wa kike wanafikia ndoto zao na kuacha tabia ya kuwaozesha wangali wadogo kwa kuwa katika umri huo hawawezi kuhimili mikimiki ya ndoa.


Mkuu wa wilaya ya Nyamagana Amina Makilagi akiongea na Wazazi na Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Mkuyuni ya jijini Mwanza.

Amesema baadhi ya sababu zinazochangia watoto wengi kuharibikiwa maishani ni pamoja na wazazi wote wawili kushindwa kutenga muda wa kulea watoto tangu wanapokuwa wadogo ili kuwajengea msingi imara utakaowasaidia maishani mwao.

“Kama kweli tunataka kuwa na kizazi kisichokuwa na kasoro niwaombe wazazi wenzangu tuwekeze muda mwingi kwa Watoto wetu hii itatusaidia kujua matamanio yao,matatizo yao na sisi kama wazazi sasa tutakuwa na wajibu wa kuwasaidia kufikia ndoto zao na hata kutatua changamoto zao”.alisema Makilagi.


Baadhi ya walezi wa Mkuyuni wakifatilia hotuba ya mkuu wa wilaya ya Nyamagana Mheshimiwa Makilagi.

Makilagi amesema wazazi wanatakiwa kuwa makini pia kwa watoto wao wa madarasa ya awali ambao mara nyingi huzua sababu za kutokwenda shule hali ambayo ikiachwa itasababisha watoto hao kuwa watoro wakubwa kwa siku za usoni.

“Mtoto anaamka asubuhi anasikia baridi anakuambia mama kichwa kinauma na mzazi bila kufikiria unamwambia lala lala mwanangu hapo humsaidii mtoto bali unatengeneza bomu”.alisema Mkilagi.

Amesema serikali inaendelea kuboresha mazingira ya elimu kwa kujenga shule bora na za kisasa kwaa ajili ya kuwapa nafasi ya kusoma watoto wote wenye sifa ya kupata elimu.


Ripoti iliyotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF mjini New York Marekani imeonya kuwa zaidi ya watoto milioni 175, yaani nusu ya watoto wote wanaotakiwa kuwa katika shule za awali kote duniani, hawasajiliwa katika elimu ya awali au chekechea na hivyo wanakosa fursa ya uwekezaji muhimu na kukosa usawa kuanzia mwanzo.

No comments